BREAKING NEWS

recent

USICHOKIJUA KUHUSU SALIM KIKEKE WA BBC


     NDUGU mpenzi msomaji au mfuatiliaji wa story hii ya sallimu kikeke wa BBC na leo tunawaletea sehemu ya pili ya story hii na hapa ndipo tulipoishia.

Kuingia utangazaji
Mara baada ya kuona matumaini yakififia kupitia taaluma yake ya kilimo, Kikeke aliamua kubadilisha ukurasa wa maisha baada ya kupiga hodi katika ofisi za kituo cha TV cha CTN ambacho kilikuwa na redio wakati huo ikijulikana kama Classic FM ambayo kwa sasa ni Magic FM.
Sababu, nia na ujasiri wa kuchukua uamuzi huo, haikutokea kama ajali, bali ilitokana na ushawishi aliokuwa ameupata kutoka kwa mama yake mzazi ambaye ni marehemu kwa sasa.

“Mama yangu alikuwa wa kwanza kunijengea uwezo wa kuingia katika utangazaji, alikuwa anapenda sana kusikiliza habari za redioni na alinishawishi kufuatilia kila habari iliyokuwa inaendelea duniani, nikawa na uwezo wa kutamka maneno vizuri na kusoma habari,” anasema Kikeke.

Ilikuwa ni mwishoni mwa 1997, Kikeke alifika katika ofisi za kituo cha kurusha matangazo  cha CTN. “Kwa sasa wanaita Magic FM, walikuwa wanafungua kituo kipya cha Classic FM hivyo niliomba kufanya kazi bure, nikapewa kipindi cha kucheza miziki ya Kiingereza,” anasema Kikeke.

Jambo la kujifunza
Jambo la kujifunza hapa ni kwamba wakati mwingine katika kusaka ajira, kubali kufanya kazi bila ya malipo, onyesha jitihada zako, huenda ikawa ni njia nzuri ya kuajiriwa katika maeneo mbalimbali yakiwemo yale ambayo huenda mtu amekwenda kwa ajili ya masomo kwa vitendo.

Njia sahihi ya kukaa katika ajira usiyo na ujuzi nayo
Anasema baada ya kupata uhakika wa kuendelea na kazi hiyo, Januari mwaka 1998, Kikeke aliamua kwenda kusoma kozi fupi ya Utangazaji habari katika chuo cha uandishi wa habari cha ‘Tanzania School of Journalism (TSJ)’.

”Pale nilisoma cheti kwa miezi mitatu na kurudi tena kazini, nikaanza kusoma habari za kiingereza na Kiswahili wakati mwingine nilikuwa naenda kutafuta habari,” anasema Kikeke.

Mafanikio yameanza kuja, lakini ghafla anafukuzwa kazi!
“Hata hivyo mwezi mmoja baadaye  wakanifukuza kazi kwa sababu ambazo nisingependa kufafanua zaidi,” anasema.

Wakati mwingine hata baya lina uzuri wake
Kikeke baada ya kufukuzwa kazi, hakuishia kulia mtaani, badala yake alianzisha mkakati wa kusaka ajira tena kwenye taasisi yenye hadhi ya juu zaidi, Radio Tanzania (RTD) ambayo sasa ni Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), hiyo ilikuwa ni mwishoni mwa mwaka 1998.

”Kwa kipindi hicho Abdul Ngarawa alikuwa mkurugenzi wa RTD, nikapelekwa idhaa ya Kiingereza,  ‘English Service’, na kuandaa vipindi vya muziki kila siku kuanzia saa 12:00 jioni mpaka saa 6:00 usiku,” anasema Kikeke na kufafanua kuwa alikuwa akifanya kazi kwa muda ‘part-time.

Alianza kupangiwa vipindi vya kutangaza baada ya kukaa  kwa zaidi ya mwaka mmoja. “Baadaye nikapewa kipindi cha Mwelekeo kilichoanzishwa wakati wa maandalizi ya kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2000, nilikuwa mtangazaji wa mwanzoni kabisa katika kipindi hicho,” anasema Kikeke.
Katika kipindi hicho, Radio Tanzania walianzisha kituo cha matangazo cha FM, kiitwacho PRT kikitoa matangazo kwa lugha  ya Kiingereza.

RTD na Kituo cha PRT ndizo kwa sasa zinafahamika kama TBC na TBC1. “Mimi nikaondoka pale na kurudi tena CTN,” anasema.

Kurudi CTN
Baada ya kurudi katika kituo hicho, Kikeke alifanikiwa kupata nafasi ya kusoma habari kwenye TV mpaka mwezi Agosti wakati kampuni hiyo ilipouzwa na kuwa chini ya kituo cha Channel Ten na DTV. Baadae alihamia ITV.

Kuingia ITV/Radio One
Baada ya hapo alifanikiwa kuandika barua ya maombi ya kazi katika Kituo cha Radio One.
“Kwa wakati huo Charles Hilary ndiye alikuwa Mkuu wa Kitengo cha Radio One, akaniomba nimpatie mfano (Demo) ya kipindi chochote nilichowahi kufanya, kwa bahati mbaya sikuwa na ya radio ila nikawa na ya TV”, anasema Kikeke.

Anaongeza kuwa hali hiyo ikamfanya abadilishe mlango wa kutoka Redio One na kuingia ITV. “Charles Hilary akaipeleka ile demo upande wa televisheni ya ITV, kulikuwa na Betty Mkwasa na Joyce Mhaville, wakaipenda kazi yangu na kuagiza niripoti pale kazini,” anasema.

Kikeke alipangiwa jukumu la utangazaji wa vipindi vya taarifa za habari kila siku na habari za ‘Jiji Letu’ hata hivyo mambo yalibadilika kwa muda mfupi pale ofisini.

Safari ya BBC
Radio One walikuwa ni Redio washirika wa BBC hivyo walikuwa na mkataba wa kuchukua mtangazaji mmoja kila mwaka na kumpeleka kufanya kazi makao makuu ya BBC kwa muda wa miezi kadhaa.
Anasema Mwezi Mei 2003 nikafaulu majaribio ya kuingia BBC, ambako anaendelea hadi leo.

Familia yake

Kikeke ni mtoto wa pili kati ya watoto watatu. Ni baba wa mtoto mmoja ambaye anasoma darasa la saba nchini. “Huku London ninaishi peke yangu,” anasema.

tumefikia mwisho wa story hii. source. mwananchi.co.tz
USICHOKIJUA KUHUSU SALIM KIKEKE WA BBC Reviewed by mudy mandai on 12/14/2015 01:03:00 PM Rating: 5

No comments:

All Rights Reserved by habartz © 2014 - 2015
Designed by JOJOThemes

Contact Form

Name

Email *

Message *

HABARI NA MATUKIO YA KIJAMIII. Powered by Blogger.