BREAKING NEWS

recent

BREAKING NEWZZZZZ; RAIS MAGUFULI ATANGAZA BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI

Watanzania wamekuwa na hamu kubwa ya kujua baraza la mawaziri, baada ya kusubira kwa muda mrefu,lakini leo Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli ameamua kutangaza baraza lake la mawaziri.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo Rais Magufuli alisema "tuliona angalau tujiridhishe kwanza, baraza lililopita lilikuwa na mawaziri na manaibu zaidi ya 59, tukaona tuwe na baraza dogo. Hatuwezi kukaa bila baraza, katika baraza hili, wizara nyingi tumeziunganisha na kutakuwa na wizara 18 na tutakuwa na mawaziri 19 tu, kuna baadhi ya wizara zitakuwa na mawaziri na hazitakuwa na manaibu waziri. "

Katika hatua nyingine Rais Magufuli alisema "Lengo ni kutimiza ahadi yetu ya kuwa na baraza dogo kupunguza gharama na effective kwa kufanya kazi. Zilitengwa bilioni 2, mawaziri watakapoteuliwa waende semina elezi, baraza nitakaloliteua halitakuwa na semina elekezi na fedha tutaelekeza sehemu nyingine kama ni madawati au kwenye elimu bure. Watafanya semina elekezi wenyewe ndani kwa ndani."

WIZARA
Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora: Mawaziri ni George Boniface Taguluvala Simbachawene na Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki, Naibu waziri Selemani Saidi Jafo.

Ofisi ya makamu wa Rais, muungano na mazingira: Waziri ni January Yusuf Makamba, naibu Luhaga Mpina

Ajira, walemavu: Jenista Joakim Mhagama, Naibu nimemtua mbunge, Abdallah Possi. M ambae ni mhadhiri Dodoma

Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi Vijana, Ajira na Walemavu: Waziri ni Jenista Muhagama, manaibu Anthony Mavunde, Possy Abdallah.

Kilimo, mifugo na uvuvi: Waziri ni Mwigulu Lameck Nchemba, naibu William Ole Nasha

Ujenzi, uchukuzi na mawasiliano: Waziri bado sijamtafuta, naendelea kumfikiria, Naibu waziri mhandisi Edwin Ngonyani.

Fedha na mipango:
 Waziri bado tunamtafuta, naibu waziri ni Ashantu Kizachi

Nishati na madini: Waziri ni Professa Sospeter M. Muhongo, Naibu waziri ni Medalled Karemaligo

Katiba na sheria: 
Waziri Harrison George Mwakyembe

Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa: Waziri ni Augustine Philip Mahiga ambae nimemteua kuwa mbunge na kisha waziri, Naibu ni Dr Suzan Kolimba.

Ulinzi na kujenga taifa: Waziri ni Dr. Hussein Ali Mwinyi

Mambo ya ndani:
 Charles Muhangwa Kitwanga

Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi: Waziri ni William Vangimembe Lukuvi, Naibu Angelina Mabula

Maliasili na Utalii: Waziri bado, naibu ni Ramo Makala

Viwanda, biashara na uwekezaji: Waziri Charles John Poul Mwijage

Elimu,Sayansi Teknolojia na Ufundi: Waziri bado hajapatikana, Naibu ni Stella Manyanya

Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto: Waziri Ummy Ally Mwalimu, Naibu ni Hamisi Andrea Kigwangalla

Habari, utamaduni, wasanii na michezo: Waziri Nape Nnauye, naibu Anastazia Wambura

Wizara ya maji na umwagiliaji: Waziri Makame Mnyaa Mbarawa ambae nilimteua kuwa mbunge, Naibu ni Isack Kamwela
BREAKING NEWZZZZZ; RAIS MAGUFULI ATANGAZA BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI Reviewed by habarinamatukioyakijamii.brogspot.com on 12/10/2015 03:59:00 PM Rating: 5

No comments:

All Rights Reserved by habartz © 2014 - 2015
Designed by JOJOThemes

Contact Form

Name

Email *

Message *

HABARI NA MATUKIO YA KIJAMIII. Powered by Blogger.