ZITTO KABWE ATAKA MSHINDI AAPISHWE ZANZIBAR
Mbunge mteule wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya Chama Cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe amefunguka na kusema kuwa matokeo ya uchaguzi wa Zanzibar yatangazwe na mshindi aapishwe.Zitto Kabwe amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Facebook na kudai kuwa suala la Zanzibar lisidharauliwe kabisa kwani hawawezi kutazama Katiba ikikanyagwa, vinginevyo amesema Maalim Seif apate Jaji amwapishe na aunde Serikali mara moja.
"Suala la Zanzibar lisidharauliwe kabisa. Matokeo yatangazwe na mshindi aapishwe. Hatuwezi kutazama tu Katiba inakanyagwa. Vinginevyo Maalim Seif apate Jaji amwapishe na aunde Serikali mara moja na kuanza kuwatumikia Wazanzibari, Serikali ya Umoja wa kitaifa kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar" Amesema Zitto Kabwe
ZITTO KABWE ATAKA MSHINDI AAPISHWE ZANZIBAR
Reviewed by habarinamatukioyakijamii.brogspot.com
on
11/10/2015 08:11:00 AM
Rating:
Reviewed by habarinamatukioyakijamii.brogspot.com
on
11/10/2015 08:11:00 AM
Rating:

No comments: